Monday 5 December 2016

UNGEKUA WEWE UNGEFANYAJE

UNGEFANYA NINI? Mwanamke alimkimbia mumewe na akamuachia mtoto mwenye miaka mitatu. Sababu kubwa ya kumkimbia mumewe ni kwamba alipata boyfriend mwenye hela ambaye alikuwa akiishi Michigan huko Marekani. Huyo Boyfriend au mchepuko wake walijuana kupitia mitandao ya kijamii. Walizoeana sana na mwisho yule boyfriend wake akamuahidi kumtafutia viza ya kuishi Marekani. Na kweli baada ya miezi kadhaa yule mwanamke alimtoroka mumewe na kutokomea Marekani, huku akiacha taarifa kwamba asitafutwe tena, anaenda kuanza maisha mengine mapya. (mumewe alifirisiwa kutokana na kutuhumiwa ubadhirifu wa mali za kampuni alikokuwa akifanya kazi). Kutokana na msongo wa mawazo na upweke kwa kipindi kirefu tokea mkewe amtoroke, yule mwanaume akaamua kuoa mke mwingine. Kwa bahati mbaya yule mwanamke mwingine aliyeolewa hakuweza kushika mimba. Hata hivyo yule mwanamke mwingine alimtunza vema mtoto wake wa kambo kama mwanae vile. Miaka michache baadae, yule mume alifariki kwa ajali ya gari alilokuwa akisafiri nalo kwenda kijijini kufanya biashara ya mazao. Mke wake wa pili alifanya kila jitihada kwa uwezo wale wote kumsomesha yule mtoto, na Mungu hakunyimi vyote kwani yule mtoto alikuwa na uwezo mkubwa wa kiakili. Mwanamke aliuza nyanya sokoni, alitembeza ndizi, alichoma mahindi barabarani na kadharika ilimradi aweze kujitunza yeye na yule mtoto wake wa kufikia. Yule mtoto alijua kwamba yule ndiye mama yake halisi na ndiye aliyekuwa akimuita mama. Mama yake halisi aliyetorokea Michigani, Marekani, hakuwahi hata siku moja kutuma salamu au kuwasiliana na mtoto wake, ingawa alipata habari kwamba mumewe wa zamani alifariki kwa ajali. Miaka mingi ilisonga na kijana alikuwa kwa akili na kimo, alikuwa Chuo kikuu akisomea Uhandisi wa mafuta na gesi (Bachelor of science in petroleum Engineering). Mama yake halisi aliyeko Marekani hakuweza kupata mtoto tena na yule mwanaume mwingine aliyemuoa, na kwa hilo yule mume wake mpya aliamua kumtimulia mbali. Kwa kutambua kuwa alifanya kosa kumkimbia mwanae, aliamua kurudi nyumbani kumtafuta mwanae na kumkabidhi utajiri alioupata akiwa Marekani (gawiwo la nusu kwa nusu la mali baada ya kutalikiana na mumewe wa Marekani) Bahati mbaya alifika na kumkuta mwane akipigania kati ya uhai na kifo kutokana na kufeli kwa figo zake. Madaktari walikuwa wakihitaji pesa nyingi kwa ajili ya upasuaji, pesa ambazo mama yake wa kambo alishindwa kabisa kuzipata. Mama yake halisi kutoka Marekani aliingilia hilo suala na kulipa pesa zote za hospitali kwa ajili ya matibabu, pia akatoa figo yake moja na maisha ya kijana yakawa yameokolewa. Baada ya matokeo ya mwisho ya chuo kikuu kutoka, kijana alipata ufaulu wa hali ya juu (first class degree) na akapewa ufadhili wa kwenda kusomea shahada ya uzamivu (masters) na baada ya hapo udaktari wa falsafa (phd) huko Burnley, Uingereza. Katika kupokea cheti chake siku ya mahafali chuoni kwao, makamu mkuu wa chuo alimpa kipaza sauti kijana na kumwambia amuite mama yake katika stage na kupokea cheti cha heshima. Baada ya makamu mkuu wa chuo kusema hayo, mama yake halisi aliyemkimbia alisimama na kujiweka sawa kusubiri kuitwa na mwanae, wakati mama yake wa kambo aliyemlea tokea mdogo akiwa bado amekaa huku machozi mengi yakimtoka huku akimuangalia mwanae wa kufikia kule mbele. Jibu naliacha hewani......................... Fikiria wewe ndio huyo mtoto, utamuita nani aje kule stejini kupokea hicho cheti? A) Mama wa kambo B) Mama mzazi Nahitaji majibu yenu, kama huna share kwa wengine waje na majibu.

No comments:

Post a Comment

Show your comments here

SHARE KWA MARAFIKI ZAKO HAPA

Popular Posts