Friday 27 January 2017

Kisa cha kusisimua

Binti wa miaka 19 ambaye aliacha shule baada ya baba na mama kufa katika ajali mbaya na ndugu kutompa msaada aliamua kuondoka nyumbani na kwenda kuishi na kijana mmoja. Miaka 10 sasa amekuwa anakaa na rafiki yake wa kiume avutaye bangi katika ghetto. Amekuwa anapewa fedha kidogo kutoka kwa huyo mpenzi wake ili anunulie chakula na kula na marafiki wa kaka huyo baada ya kutumika kimapenzi kwa wiki zima huku akiuza maji ya kunywa. Baada ya muda akajikuta ni mjamzito na huyo kijana akamwambia watoe tu mimba hiyo.Akampa fedha kidogo na kumwambia aongeze nyingine ambazo amekuwa akimpa ili akatoe mimba bila kukumbuka kuwa fedha hizo zimekuwa zikitumika kwa ajili ya chakula. Siku ya pili yake akiwa anatoka chumbani mwao kwenda kutoa mimba, akpita kwenye korido ambako akakanyanga sakafu ambayo ina maji na kuteleza. yule kijana akamwona wakati anaangukia tumbo pale sakafuni na akasema, “ amini au usiamini hii ndio njia rahisi niliyoitaka uitumie kutoa mimba hiyo” Kijana akamchukua binti wakati huo damu nyingi zikimtoka na kumwambia aende bafuni akanawe.Lakini kwa nguvu za mwenyezi Mungu yule dada alipona ingawa mimba ilitoka na akaumwa kwa zaidi ya wiki bila msaada wowote ule.. Siku moja akiwa anauza maji akakutana na muuza magazeti na kumpa maji pakiti moja bure na kumwambia, “leo ni miaka kumi tangu baba na mama yangu wafariki katika ajali mbaya, hivyo sitajali mchumba wangu atasemaje au kunifanya nini kwa kutoa maji haya bure, ila mimi nitatoa maji bure kama kumbukumbu ya siku hii yenye simanzi kwangu”. Akiwa anataka kuondoka yule muuza magazeti akamwambia kuwa kuna nafasi ya kazi sehemu na kuwa atamsaidia kuandika barua ya kuomba. Yule dada ailishukuru na akawa anampigia mara kwa mara yule muuza magazeti mpaka siku akaitwa kwenda kwenye usaili. Siku ya usaili akiwa njiani anaelekea huko akakutana na mama mmoja akiwa na gari aina ya BMW likiwa nimeishiwa mafuta. Yule dada akamuuliza mama, Je unahitaji msaada gani? yule mama akamwambia nimeishiwa mafuta na sijui cha kufanya hapa. Dada akachukua kidumu na kwenda mbio kumnunulia mafuta yule mama na akarudi na kumpa. Yule mama alipotaka kumpa hela, dada akakataa akasema nimekuona nikamkumbuka mama yangu hivyo nimefurahi kukusaidia, kama hutajali naomba niwahi sehemu. Kufika kwenye usaili dada akashangaa kuona kumbe yule mama mwenye BMW ndio boss wa ile kampuni na akafanyiwa usahili na kuanza kazi na sasa anajimudu kifedha na ana biashara zake. Na sasa hakai tena na yule kijana mvuta bangi wakati nusu ya utajiri wake anaupeleka kwenye vituo vya kulelea watoto yatima. Nami leo nakuombea unayeisoma habari hii, Mungu akujalie na kukufungulia milango ya mafanikio katika kila jaribu unalolipitia na ukumbuke kuwasaidia wanao hitaji msaada wako. Comment neno “Amen” na kisha share Huwezi jua madhara ya kuupuuzia ujumbe huu

No comments:

Post a Comment

Show your comments here

SHARE KWA MARAFIKI ZAKO HAPA

Popular Posts