Sunday 2 October 2016
SISI WANAUME BHANA...
Mwanaume mmoja aliwatongoza wanawake watatu
tofauti na nia yake ni kufanya upembuzi yakinifu
ili mmoja wao awe mkewe. Hivyo jamaa aliamua
kuwapa jaribio kwa kuwapa Tsh. 500,000/= kila
mmoja huku akitaka kujua ni namna gani
watazitumia.
Mwanamke wa kwanza alitumia pesa yote kununua
vipodozi. Alitembelea duka la vipodozi na urembo
akajikwatua sawa sawa na kubust makalio!
Alivyorudi kwa mchumba wake akamwambia,
"Nimeamua kutumia pesa yote kwa ajili ya
kujipamba ili nizidi kukupendeza
machoni pako na kukuvutia maana nakupenda
sana."
Hakika yule mwanaume akapendezwa sana na
mpenzi wake.
Mwanamke wa pili alinunua zawadi kwa ajili ya
bwana wake. Alinunua simu janja mpya kwa ajili
ya bwana wake, saa ya kisasa, nguo na viatu
vizuri. Alivyofika kwa bwana wake alimwambia,
"Pesa yote nimeitumia kununua hizi zawadi zako
maana nina kupenda sana."
Jamaa akafarijika sana
Mwanamke wa tatu aliwekeza zile pesa kwenye
soko la hisa na baada ya muda fulani alipata faida
ya shilingi 2,000,000/=. Mwanamke yule aliamua
kumrudishia bwana wake ile pesa aliyokuwa
amepewa yaani laki 5 na pesa iliyokuwa imebakia
alifungua akaunti ya pamoja na bwana wake.
Kisha yule mwanamke akamwambia yule jamaa,
"Nahitaji kuwekeza na kuhifadhi kesho yetu kwa
sababu nakupenda sana."
Hakika yule mwanamke alimfurahisha sana jamaa.
Jamaa akatafakari sana yale ambayo yalikuwa
yamefanywa na wale wanawake baada ya kupewa
laki 5. Lakini mwisho wa siku jamaa aliamua
kumwoa mwanamke mwenye makalio makubwa!
*Wanaume hatupendag ujinga sisi* 😂😂😂😂
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
SHARE KWA MARAFIKI ZAKO HAPA
Popular Posts
-
INTRODUCTION This work has contain four parts which are introduction that consist of meaning of the key terms, historical background of Leop...
-
Question: Discuss the role of Delegated Legislation in ensuring smooth administrative functions in Tanzania. 1.0 Introduction This work is...
-
INTRODUCTION. This document contains the definition of key terms which are natural justice, principle of natural justice andadministrative t...
-
COMMUNICATION AND INFORMATION SYSTEMS COMMUNICATION It is obvious fact that communication is such vital part of each of us that it contribut...
No comments:
Post a Comment
Show your comments here